Wednesday, July 31, 2013

WEWE NI NURU YA ULIMWENGU.

Ewe Mkristo; wewe ni NURU YA ULIMWENGU (Mathayo 5:14). Hivyo basi; ili uweze kuuangazia ulimwengu unapaswa kufanya hivi:
"Yatendeni mambo yote pasipo manung'uniko wala mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu." ~ WAFILIPI 2:14-15.
Ni kweli kwamba sisi tumo ndani ya kizazi kilichopotoka na chenye ukaidi; hatumo humu kwa mkosi bali ni kwa kusudi la Mungu ili sisi tuuangazie ulimwengu wapate kumjua Mungu kupitia sisi. Mungu anataka sisi tuufikie ulimwengu usiomjua Yeye ili tuubadilishe upate kumjua na kumpokea Yeye.

Ewe mtumishi wa Mungu, hakikisha mahali pote ulipo unauangazia ulimwengu kwa neno la Mungu na maisha matakatifu. Sisi tumeokolewa ili tuujenge mwili wa Kristo. Mtangaze Yesu kila mahali ulipo, hiyo ndiyo kazi tuliyoamriwa tuifanye. Kuhubiri ni amri wala si ihari; Yesu anasema kwamba;
"...nimewapa AMRI ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru." ~ LUKA 10:19
Kila Mkristo analazimika KUHARIBU KILA KAZI YA SHETANI, endapo kama usipofanya hivyo unakuwa umekaidi kutii AMRI hiyo. USIOGOPE kwa sababu Yesu ametuambia:
"...hakuna kitu kitakachowadhuru." ~ LUKA 10:19
Nawatakieni huduma njema na yenye baraka tele iliyojawa na nguvu na uweza wa Roho Mtakatifu. Ukimwamini Yesu na ukimwacha Yeye akuongoze; hakika yote yawezekana katika jina la Yesu.

0 MAONI:

Post a Comment

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii