MASHARTI

sparkle effect

MASHARTI YA UTUMIAJI TOVUTI HII.


Imetolewa: Mei 13, 2013

Karibu kwenye huduma ya Neno La Uzima.

Asante kwa kutumia huduma hii ya Neno La UZIMA. Huduma hii imeanzishwa nami Mwinjilisti Masanja C. Sabbi. Mimi ni Mkristo niliyebatizwa kwa maji mengi na kwa Roho Mtakatifu. Ni Mwafrika, Mtanzania ninayeishi nchi ya Tanzania (Afrika Mashariki) katika jiji la Mwanza.
Pindi utumiapo huduma hii, unakuwa umekubaliana na masharti yafuatayo. Tafadhari yasome kwa umakini mkubwa sana. Pia masharti haya yanaweza kuboreshwa kulingana na uhitaji pamoja na ulazima wa kufanya hivyo.

Utumiapo Tovuti Hii:

Ni lazima ufuate masharti yote yaliyowekwa ndani ya huduma hii.
Kamwe usiitumie vibaya huduma hii (tovuti hii). Kwa mfano,
Ø       Usinakili cho chote kilichomo ndani ya tovuti hii kwa lengo la kufanyia biashara au kujipatia maslahi binafsi pasipo kupewa idhini ya mmiliki wa tovuti hii. Unaruhusiwa ku-“share” mafundisho haya kwa rafiki zako (nyumbani, shuleni, chuoni, kazini, katika jamii, n.k.) kwa njia ya kusoma moja kwa moja katika tovuti hii, au kwa njia ya kuwatumia masomo hayo kwa barua pepe, au kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii; lakini, ni marufuku kunakili kazi hii na kwenda kuifanyia biashara kwa namna yo yote ile.
Ø       Ni marufuku kutumia lugha ya matusi aidha kwa kutuma maoni (comment) kwenye mada mbalimbali zilizomo ndani ya tovuti hii, au kwa ujumbe wo wote wa barua pepe, au kwa kutumia mitandao ya kijamii, au kwa simu, wala kwa njia ya namna yo yote ile. Endapo ukikiuka masharti haya; taratibu za kisheria zitachukua mkondo wake.
Kila mtu mtumiaji wa tovuti hii anao uhuru wa kuchangia mada yo yote ile au kuweka maoni kwa uhuru pasipo kukiuka masharti hayo hapo juu. Pia Biblia Takatifu inatuagiza kuyaheshimu mamlaka yaliyopo hapa duniani kwa maana Mungu ndiye ameyaruhusu kuwepo (Warumi 13:1-7). Kuheshimu mamlaka maana yake ni kutii kile ambacho hakipingani na neno la Mungu.
Sasa basi; kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 toleo la mwaka 2005 (Nanukuu Katiba ya Tanzania kwa kuwa huduma hii imeanzia katika ardhi ya Tanzania japokuwa huduma hii ni kwa watu wote). Nanukuu baadhi ya vipengere katika “SEHEMUI YA TATU” ya Katiba hiyo inayohusu “HAKI NA WAJIBU MUHIMU."
Nanukuu:
“Haki ya uhuru wa mtu binafsi Sheria ya 1984 Na.15 ib.6
15.-(1) Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru.”
“Haki ya Uhuru wa Mawazo. Uhuru wa maoni Sheria ya 2005 Na.1 ib.5
18. Kila mtu-
(a)    anao uhuru wa kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(b)    anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila ya kujali mipaka ya nchi;
(c)    anao uhuru wa kufanya mawasiliano na haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake; na
(d)  anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa  maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii.
19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja    na uhuru wa mtu kubadili dini au imani yake.
(2) Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
(3) Hifadhi ya haki zilizotajwa katika ibara hii itakuwa chini ya taratibu zilizowekwa na sheria ambazo ni muhimu katika jamii ya kidemokrasia kwa ajili ya usalama wa jamii, amani katika jamii, maadili ya jamii na umoja wa kitaifa.
(4) Kila palipotajwa neno “dini” katika ibara hii ifahamike kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno mengineyo yanayofanana au kuambatana na neno hilo nayo yatatafsiriwa kwa maana hiyo.”
Mwisho wa kunukuu.
Pindi utumiapo huduma hii (Neno La UZIMA) unakuwa umekubali kutii Katiba hiyo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kwa mwongozo wa nukuu hizo hapo juu).

Shukurani:

Baada ya hayo; napenda kutoa shukrani za dhati kwa kutembelea tovuti hii, na pia ninaamaini umesoma masharti hayo na umeyaelewa. Tendo la kuendelea kutumia tovuti hii linamaanisha kuwa umekubaliana na masharti hayo na hakika unayatekeleza.
Katika huduma hii ya Neno la UZIMA hatubagui dini wala imani ya mtu. Upo huru kuchangia mawazo yako pasipo kuvunja Sheria, Masharti pamoja na Taratibu zilizowekwa.
Kumbuka wajulishe ndugu, jamaa, na marafiki ili nao waje wajifunze neno la Mungu kupitia huduma hii.
Ni mimi mtumishi wa Mungu,    
             Mwinjilisti Masanja Sabbi.
Mwenyezi Mungu akubariki katika jina la Yesu Kristo, amina.

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii