
SALA / MAOMBI
Hili ni
tendo ambalo watu wanaoamini humwendea Mungu wakimwabudu, wakifanya toba,
wakimshukuru na kumwomba mambo mbali mbali. Sala / Maombi ni mawasiliano ya
moja kwa moja kati ya mtu anayeamini na Mungu. Unamweleza Mungu kile kilichomo
ndani yako (hatuombi kwa kukariri bali
tunasema kile kilichomo ndani yetu); yanaweza kuwa ni sala / maombi binafsi
au maombezi kwa ajili ya wengine.
Tunaposoma
Biblia katika Injili ya Luka 11:1, mwanafunzi wa Yesu anamwambia Bwana wake
kwamba:
“…Bwana, tufundishe sisi kusali…”
– Luka 11:1
Kuna jambo
la kuzingatia hapa: Kabla ya kuingia katika maombi, ni muhimu sana kutambua kwanini
tunaomba,...