Sunday, January 28, 2018

BWANA, TUFUNDISHE SISI KUSALI (Luka 11:1)

SALA / MAOMBI Hili ni tendo ambalo watu wanaoamini humwendea Mungu wakimwabudu, wakifanya toba, wakimshukuru na kumwomba mambo mbali mbali. Sala / Maombi ni mawasiliano ya moja kwa moja kati ya mtu anayeamini na Mungu. Unamweleza Mungu kile kilichomo ndani yako (hatuombi kwa kukariri bali tunasema kile kilichomo ndani yetu); yanaweza kuwa ni sala / maombi binafsi au maombezi kwa ajili ya wengine. Tunaposoma Biblia katika Injili ya Luka 11:1, mwanafunzi wa Yesu anamwambia Bwana wake kwamba: “…Bwana, tufundishe sisi kusali…” – Luka 11:1 Kuna jambo la kuzingatia hapa: Kabla ya kuingia katika maombi, ni muhimu sana kutambua kwanini tunaomba,...

Thursday, January 11, 2018

JIONESHE KUWA MWANAMUME

 JIONESHE KUWA MWANAMUME (1 Wafalme 2:1) Bwana Yesu Kristo apewe sifa. Ninamshukuru Mungu kwa neema Yake kuu amenipatia kibali cha kulihudumia kanisa Lake hata sasa. Leo ninao ujumbe wenye baraka kwako uliobeba kichwa kinachoitwa: JIONESHE KUWA MWANAMUME. Huu ni mwanzoni mwa mwaka 2018, watu wengi wanatazamia baraka nyingi ziambatane nao; hivyo basi, Roho wa Mungu amenipa ujumbe huu kwa ajili yako: “JIONESHE KUWA MWANAMUME”. Hebu tufungue Biblia zetu tusome 1 Wafalme 2:1-2, Biblia Takatifu inasema: “Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema, Mimi naenda njia ya ulimwengu wote (yaani, naenda kufa);...

Wednesday, April 19, 2017

THAWABU YANGU NI NINI?

NAWAKUMBUSHA TU WATUMISHI WA MUNGU "Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila gharama..." - 1 Kor 9:18 Inawezekana andiko hili huwa unalipita au haujawahi kulisoma; lakini leo napenda kukukumbusha mtu wa Mungu, kabla ya kuingia kwenye huduma, ni vema ukazingatia andiko hili. Mbarikiwe sana watu wa Mun...
Page 1 of 712345Next

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii