Saturday, October 4, 2014

UZIMA NA MAUTI VIPO MBELE YAKO, BARAKA NA LAANA ZIPO MBELE YAKO. UCHAGUZI NI WAKO ! ! !

SIRI YA KUANGAMIA IPO HIVI:

~ TENDA DHAMBI

~ KAIDI NENO LA MUNGU

~ SHIKA MAPOKEO YANAYOPINGANA NA NENO LA MUNGU
(Mfano; Neno la Mungu linapokwambia: "USIIBE" wewe iba; ukiambiwa "USIZINI" wewe zini; ukiambiwa "USISEME UONGO" wewe sema uongo; Ukiambiwa: "USIOMBE WAFU" wewe omba wafu; ukiambiwa: "YESU NI MUNGU" wewe kataa; ukiambiwa "USIABUDU SANAMU" wewe abudu; ukiambiwa: "USIUE" wewe ua!

Kweli nakuhakikishia kabisa ukifanya hivyo UTAANGAMIA; kwa sababu neno la Mungu linatuambia hivi:
 "Bali WAOGA, na WASIOAMINI, na WACHUKIZAO, na WAUAJI, na WAZINZI, na WACHAWI, na hao WAABUDUO SANAMU, na WAONGO WOTE, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti..." ~ UFUNUO 21:8
HIYO NDIO SIRI YA KUANGAMIA. ANGAMIA UKIWA UNAJITAMBUA KABISA UNAANGAMIA, NA MWISHO WAKO UTATUPWA KATIKA ZIWA LA MOTO WA MATESO YA MILELE.

ZINGATIA HILI: HAKUNA NEEMA BAADA YA KIFO; HAKUNA MAOMBI YA KUMWOKOA MTU ALIYEKUFA KATIKA DHAMBI; HAKUNA UTAKASO WA DHAMBI KWA MFU !

NAYO SIRI YA UZIMA WA MILELE IPO HIVI:


TUBU SASA!
UPOKEE WOKOVU MAANA NEEMA BADO INGALIPO, MKIRI YESU AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO, BATIZWA NA USHIKE KILA NENO ALILOTUAMURU YESU TULIFANYE. UKIFANYA HIVYO UTAKUWA NA UZIMA TELE, TENA UZIMA WA MILELE.
UCHAGUZI NI WAKO, KWA MAANA NENO LA MUNGU LINATUAMBIA HIVI:
"Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako;
kumpenda BWANA, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako..."
~ KUMB 30:19-20
UZIMA NA MAUTI VIPO MBELE YAKO, BARAKA NA LAANA ZIPO MBELE YAKO.

UCHAGUZI NI WAKO ! ! !

0 MAONI:

Post a Comment

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii