Monday, August 11, 2014

"Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote..." ~ WAKOLOSAI 3:16

"Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote..." ~ WAKOLOSAI 3:16

Kama jinsi mwili unavyoweza kudhoofika kwa kukosa chakula bora; vivyo hivyo na roho yako idhoofikavyo kwa kukosa neno la Mungu. Kama jinsi urafiki kati ya mtu na mtu unavyoweza kuvunjika kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara; vivyo ndivyo kukosa sala na maombi kunaifanya roho yako ijitenge mbali na Mungu.

Watu wengi wapo bize (busy) katika shughuli zao hata wanamsahau Mungu; Je, wajua kwamba shughuli zote uzifanyazo ni ubatili, isipokuwa tu kumtumikia Mungu!

Elewa kwamba; mbinguni hautaingia kwa sifa ya udaktari, kwani huko hakuna wagonjwa; mbinguni hautaingia kwa sifa ya uinjinia (uhandisi) kwani huko mbinguni miji imeshawekwa tayari na barabara zake hazibomoki; wala uanasiasa wako hauna nafasi mbinguni, kwa maana Mungu peeke ndiye Mtawala wa huko; hata ujuzi wako katika sekta ya ulinzi, upelelezi na usalama hauhitajiki mbinguni! Mbinguni hakuna nafasi za kazi ya uhakimu, uanasheria, wala uwakili, kwa maana waovu hawatakuwepo huko. Sasa wewe wajuvunia nini! Je, ujuzi wako unafaida gani endapo usipomtumikia Mungu?

Ukristo sio dhehebu, bali Ukristo ni uhusiano kati ya mtu na Mungu. Wewe umeokolewa ili ufanyike chombo cha kuwahubiria hao watu wakuzungukao; pia umeajiriwa katika kitengo hicho ulichopo ili uwe chombo cha kulifikisha neno la Mungu mahali hapo. Upo hapo kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Usiionee haya Injili, kaza mwendo, nawe utaipokea taji ya uzima kutoka kwa Bwana wetu Yesu.

Kumbuka; NENO LA KRISTO YESU LIKAE KWA WINGI NDANI YAKO. SALA NA MAOMBI NDIYO SILAHA YAKO KATIKA IMANI.

Nakutakia baraka tele.

0 MAONI:

Post a Comment

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii