Thursday, April 30, 2015

SIYO MAPENZI YA MUNGU WEWE UTESEKE!


Neno la Mungu linasema hivi:

"Je! Mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie mwana wa tumbo lake? Naam, hawa waweza kusahau, lakini Mimi sitakusahau wewe.
Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono Yangu; kuta zako ziko mbele Zangu daima." - Isaya 49:15-16

Mwanadamu anaweza kukutenga, anaweza kukunyanyasa, anaweza kukufanyia mabaya; lakini USIKATE TAMAA. Haijarishi unapitia magumu kiasi gani: iwe katika ndoa yako, iwe katika biashara yako, iwe katika uchumba wako, iwe katika afya yako, iwe katika uchumi wako, iwe katika jamii yako, iwe katika masomo yako; USIKATE TAMAA, Jibu lipo, na ipo njia ya kutokea. Mwamini Yesu TAYARI amekushindia.

Hayo magumu unayapata ili imani yako izidi kukua hata Shetani apate kuaibika kwamba tayari ameshindwa tangu pale msalabani Yesu aliposema IMEKWISHA.

Pokea jibu la mahitaji yako sasa katika jina la Yesu Kristo. Amen.

Thursday, February 26, 2015

UNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU KWA NJIA YA IMANI; HAUNA SABABU YA KUMWOGOPA SHETANI WALA KAZI ZAKE ZOTE!

Biblia Takatifu inasema kwamba:

"Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema zake nyingi alituzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye uzima kwa kufufuka kwake Yesu Kristo katika wafu; tupate na urithi usioharibika, usio na uchafu, usionyauka, uliotunzwa mbinguni kwa ajili yenu. Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho." - 1 Petro 1:3-5

Wakati umefika Mkristo kuyatambua mamlaka uliyopewa na Mungu Baba. Biblia inasema: Mungu Baba (JEHOVA / YAHWEH) ametuzaa mara ya pili ili tupate tumaini lenye UZIMA kupitia ufufuko wa Bwana wetu Yesu Kristo. Hapa zingatia sana: Tumaini hilo la UZIMA tunalipata kupitia UFUFUKO wa Yesu Kristo; hatulipati tu kupitia Yesu, bali tunalipata kupitia UFUFUKO wa Yesu Kristo. Lazima uelewe kuwa UFUFUKO wa Yesu Kristo ndio umekamilisha uzima wetu.

Hapa siongelei habari za udini, maana kuna watu wa dini ambao Yesu wao bado amekufa / yupo kaburini!
Hapa siongelei habari za Yesu wa kwenye Qur'an; Injili ni kulitangaza neno la Mungu bila unafiki wala kufichana: Issa bin Maryamu bado amekufa! Lakini Yesu Kristo Mwana wa YAHWEH yupo hai. Issa bin Maryamu alikuja kumtangaza ALLAH, lakini Yesu Kristo alikuja kutimiza mapenzi ya Baba Yake wa mbinguni anayeitwa YEHOVA. Wakristo mwe na akili; huo upuuzi wa kukubali Issa bin Maryamu unawafanya kuwaondolea mamlaka mliyowekewa na Mungu Baba ndani yenu.

Biblia inasema: KUFUFUKA kwa Yesu kunatupatia TUMAINI LA UZIMA. Sisi ni uzao mteule wa Mungu; sisi ni milki ya Mungu; YEHOVA ametuzaa mara ya pili na kutufanya sisi kuwa milki Yake. Hakuna pepo mchafu wala mchawi mwenye mamlaka juu yako ikiwa wewe umemkabidhi Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yako. WEWE UNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU KWA NJIA YA IMANI.

Hatulindwi na nguvu za Mungu kwa kuvaa rozari, wala hirizi! Huo ni utapeli tu wa kidini. Neno IMANI ni kutenda pasipo kutumia vielelezo. Nguvu za Mungu hazimo katika maji, wala vitambaa, wala sanamu, wala mafuta; bali nguvu hizo zimo ndani yetu kwa sababu sisi ni hekalu la Mungu, Roho Mtakatifu ameweka makao Yake ndani yetu, nasi tunashinda zaidi ya kushinda.

Mkristo anayejitambua haogopi wachawi wala hila za Shetani. Mkristo anayejitambua hutumia mamlaka ya jina la Yesu kwa kuharibu kila kazi za Shetani. Sisi tunaye Mungu ndani yetu; tunapokutana na upinzani wa Shetani huo huwa sio muda wa kuomba bali ni muda ya kukemea katika jina la Yesu Kristo. Mtu aliyeokoka anatambua yeye ni nani katika ulimwengu huu. SISI TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU KWA NJIA YA IMANI.

Neema hiyo ipo kwa wale tu waliomkabidhi Yesu awe Bwana na Mwokozi wa maisha yao. Kama wewe bado haujamkabidhi Yesu maisha yako; basi sali sala hii fupi:

"Mungu Baba, asante kwa wokovu ulionipatia kupitia Yesu Kristo. Ninakiri pasipo msaada wako mimi nimeangamia; sasa ninayakabidhi maisha yangu Kwako, nitakase dhambi zangu kwa damu ya Yesu Kristo; tawala maisha yangu tangu sasa, niongoze katika mapenzi Yako, nifanye niwe jinsi Wewe utakavyo niwe kwa ajili ya utukufu Wako. Ninaomba Roho Wako Mtakatifu aniongoze tangu sasa hata milele. Asante kwa kunifanya kiumbe kipya katika jina la Yesu Kristo. Amen"

Amini tayari umekuwa kiumbe kipya, amini tayari umesamehewe dhambi; lakini umebakiwa na kitu kimoja tu! Ambatana na watu (Kanisa) wanaohubiri Injili ya kweli (wokovu) ili uweze kukua katika imani.

Nakutakia baraka tele katika jina la Yesu Kristo. Amen.

Thursday, January 8, 2015

CHUKIA UMASIKINI, LAKINI WAPENDE MASIKINI. WAELIMISHE NA UWASAIDIE.

CHUKIA UMASIKINI, LAKINI WAPENDE MASIKINI. WAELIMISHE NA UWASAIDIE.

Kwa mujibu wa maono niliyonayo:

UMASIKINI maana yake ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Umasikini sio hali ya mtu kuwa na kipato chini ya dola moja, wala sio hali ya mtu kukosa mahitaji aliyonayo. Hiyo ni tafasiri mbovu ambayo watu wengi wamefundishwa na kuiweka akilini mwao. Hayo ni matikeo ya umasikini lakini sio maana halisi ya umasikini. Narudia tena:

UMASIKINI ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Watu wengi ni masikini kwa sababu wanayo BIDII KUBWA katika kuwa masikini! Wanayachukia maarifa; hawapendi kushughulisha akili zao; wanapenda kuomba omba!
Kuna wajinga wengi wanaodhani kuwekewa mikono na mchungaji ndipo watakuwa matajiri; wajinga wengine wanaambiwa panda mbegu utapata dabo dabo! Baraka za Mungu hazipo namna hiyo; bali baraka za Mungu utazipata pale unapokuwa na afya akilini mwako. Kitu cha kwanza unachopaswa kuchughulika nacho ni akili yako; uwe na fikra / mtazamo mzuri akilini mwako. Sikukatazi kutoa changizo kanisani mwako; lakini unatakiwa kuelewa kuwa Mungu leo hanashida ya kukubariki kwa sababu tayari amekwisha kukubariki; Lakini leo Mungu anahitaji uponyaji ufanyike katika akili zako ili neno Lake likae kwa wingi ndani yako na ndipo uweze kuziona, kuzifata, na kuzitumia baraka ambazo tayari amekubariki.

Ninaongea kwa maneno mmakali lakini ninaamini yanaleta uponyaji katika akili yako. Hakuna utajiri utakaoupata endapo kama hautapata uponyaji katika akili yako; uponyaji huo ni kupata maarifa. Soma vitabu sahihi, jifunze katika mitandao sahihi, sikiliza nyimbo sahihi, tazama vitu sahihi, na ujifunze kwa watu waliofanikiwa; Badiri fikra zako.

Penda maarifa.
Watu wengi wanatamani mabadiriko lakini wao wenyewe hawataki kubadirika! Haiwezekani kukokotoa hesabu kwa kanuni iliyoshindwa! Vivyo hivyo hauwezi kupata matokeo tofauti kwa kutumia mbinu ile ile iliyoshindwa! Ukifanya hivyo utafanana na mtu mpumbavu.
Mafanikio ya mtu yamo katika fikra na mtazamo wa akili alionao mtu. Mafanikio ya mtu hayapimwi kutokana na vitu aliyonavyo, wala elimu aliyonayo; bali mafanikio ya mtu yanapimwa kutokana na uwezo wake wa kufikiri akilini mwake. Watu wengi akili zao zimekufa japokuwa miili yao inaishi! Wengi wanawaza kusoma sana ili wapate vyeti vitakavyowawezesha kuajiriwa. Ndio, hayo ni mawazo mazuri, lakini sio mawazo mazuri sana. Je, usipopata ajira umejiandaa kufanya nini? Umejiandaa kulaumu serikali au umejiandaa kuwa kibaka! Au umejiandaa kuwa omba omba!

Tumia akili yako vizuri.
Ni kweli wasomi ni wengi, ni kweli ajira ni adimu, ni kweli wengi hawana mitaji; lakini tumia akili yako vizuri. Kile unachoomba watu wakusaidie, ujue nao pia wamekitafuta. Jifunze kutafuta sio kuomba omba. Pesa inakuja pale unapoiwekea mtego, mtego mzuri unatokana na fikra pevu za mtegaji. Tambua kwamba: pesa sio thamani bali ni kipimo cha thamani!

Kuna mambo matatu ambayo ni muhimu kuyazingatia; kwa mtu mwanye fikra pevu hupenda kuwa na mambo yafuatayo:

1. Haki ya kuishi.

2. Haki ya kufanya maamuzi sahihi.

3. Afya bora. [Afya ni pamoja na mwili kutokushambuliwa na maradhi wala magonjwa; Akili kuwa na fikra nzuri; pamoja na uwezo wa kifedha!]

Yote hayo utayapata pale unapokuwa na maarifa. Soma vitabu vizuri, na ujifunze kwa waliofanikiwa. Hebu fikiri zaidi ya hapo awali; badili fikra zako. Usipende kuomba omba; jifunze kuwajibika kwenye maisha yako mwenyewe. Kila mtu anawajibika katika kuyabadili maisha yake yeye mwenyewe; iwe kiroho hata kimwili. Hakuna ajira itakayokufanya uwe tajiri, hakuna serikali itakayokufanya uwe tajiri; Hiyo yote ni mifumo tu! HAKUNA MFUMO ULIOTENGENEZWA ILI UKUFANYE WEWE UWE TAJIRI; kila mfumo umewekwa kumnufaisha zaidi yeye aliyeuweka! Kama wewe akili zako zote zinategemea ajira, au serikali ikuletee utajiri; basi elewa wazi umepata ziro katika mafanikio yako! Hata kama umeajiriwa, hebu waza kuwa na mambo yako mwenyewe. Hebu nikupe siri hii itakusaidia: Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing! Najua hapo wengi hawajaelewa, narudia tena: Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing! Narudia tena kwa mara ya tatu ili uelewe vizuri:

Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing!

Sio nia yangu hasa wakati huu kukufundisha what is Network Marketing or Direct Selling, or Personal Franchise, or Mult Level Marketing Business. Ukitaka kuyajua hayo nitafute kwa muda wako; lakini kama kweli unahitaji kufanikiwa; BADILI MTAZAMO NA FIKRA ZA AKILI YAKO.

Tunahitaji uhamsho katika kanisa; akili zilizokufa tunatakiwa tuzifufue. Hebu juilize; utakuwa omba omba mpaka lini? Nani kakwambia umasikini ni kutokana na elimu ndogo au kukosa mtaji! Ukweli ni kwamba; umasikini wa mtu umo katika fikra mbaya alizonazo.

Ongeza maarifa, acha kuomba omba, chukia umasikini lakini wapende masikini; wasaidie na uwaelimishe.

Jambo la mwisho ninalopenda kukwambia, ni hili: ONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU. Pasipo Roho Mtakatifu hauwezi kumpendeza Mungu, na pasipo kumpokea Yesu hauwezi kuurithi uzima wa milele. Kila ufanyalo zingatia HAKI na KWELI.

Nimeongea mengi lakini kwa uchache sana; yatakuwa na msaada kwake yeye mwenye hekima na akili. Mungu tayari amekwisha kukubariki, tatizo limo tu kwenye akili yako! Kumbuka kwamba:

UMASIKINI maana yake ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Nawatakia baraka tele katika jina la Yesu Kristo. Amen.

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii