Thursday, January 8, 2015

CHUKIA UMASIKINI, LAKINI WAPENDE MASIKINI. WAELIMISHE NA UWASAIDIE.

CHUKIA UMASIKINI, LAKINI WAPENDE MASIKINI. WAELIMISHE NA UWASAIDIE.

Kwa mujibu wa maono niliyonayo:

UMASIKINI maana yake ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Umasikini sio hali ya mtu kuwa na kipato chini ya dola moja, wala sio hali ya mtu kukosa mahitaji aliyonayo. Hiyo ni tafasiri mbovu ambayo watu wengi wamefundishwa na kuiweka akilini mwao. Hayo ni matikeo ya umasikini lakini sio maana halisi ya umasikini. Narudia tena:

UMASIKINI ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Watu wengi ni masikini kwa sababu wanayo BIDII KUBWA katika kuwa masikini! Wanayachukia maarifa; hawapendi kushughulisha akili zao; wanapenda kuomba omba!
Kuna wajinga wengi wanaodhani kuwekewa mikono na mchungaji ndipo watakuwa matajiri; wajinga wengine wanaambiwa panda mbegu utapata dabo dabo! Baraka za Mungu hazipo namna hiyo; bali baraka za Mungu utazipata pale unapokuwa na afya akilini mwako. Kitu cha kwanza unachopaswa kuchughulika nacho ni akili yako; uwe na fikra / mtazamo mzuri akilini mwako. Sikukatazi kutoa changizo kanisani mwako; lakini unatakiwa kuelewa kuwa Mungu leo hanashida ya kukubariki kwa sababu tayari amekwisha kukubariki; Lakini leo Mungu anahitaji uponyaji ufanyike katika akili zako ili neno Lake likae kwa wingi ndani yako na ndipo uweze kuziona, kuzifata, na kuzitumia baraka ambazo tayari amekubariki.

Ninaongea kwa maneno mmakali lakini ninaamini yanaleta uponyaji katika akili yako. Hakuna utajiri utakaoupata endapo kama hautapata uponyaji katika akili yako; uponyaji huo ni kupata maarifa. Soma vitabu sahihi, jifunze katika mitandao sahihi, sikiliza nyimbo sahihi, tazama vitu sahihi, na ujifunze kwa watu waliofanikiwa; Badiri fikra zako.

Penda maarifa.
Watu wengi wanatamani mabadiriko lakini wao wenyewe hawataki kubadirika! Haiwezekani kukokotoa hesabu kwa kanuni iliyoshindwa! Vivyo hivyo hauwezi kupata matokeo tofauti kwa kutumia mbinu ile ile iliyoshindwa! Ukifanya hivyo utafanana na mtu mpumbavu.
Mafanikio ya mtu yamo katika fikra na mtazamo wa akili alionao mtu. Mafanikio ya mtu hayapimwi kutokana na vitu aliyonavyo, wala elimu aliyonayo; bali mafanikio ya mtu yanapimwa kutokana na uwezo wake wa kufikiri akilini mwake. Watu wengi akili zao zimekufa japokuwa miili yao inaishi! Wengi wanawaza kusoma sana ili wapate vyeti vitakavyowawezesha kuajiriwa. Ndio, hayo ni mawazo mazuri, lakini sio mawazo mazuri sana. Je, usipopata ajira umejiandaa kufanya nini? Umejiandaa kulaumu serikali au umejiandaa kuwa kibaka! Au umejiandaa kuwa omba omba!

Tumia akili yako vizuri.
Ni kweli wasomi ni wengi, ni kweli ajira ni adimu, ni kweli wengi hawana mitaji; lakini tumia akili yako vizuri. Kile unachoomba watu wakusaidie, ujue nao pia wamekitafuta. Jifunze kutafuta sio kuomba omba. Pesa inakuja pale unapoiwekea mtego, mtego mzuri unatokana na fikra pevu za mtegaji. Tambua kwamba: pesa sio thamani bali ni kipimo cha thamani!

Kuna mambo matatu ambayo ni muhimu kuyazingatia; kwa mtu mwanye fikra pevu hupenda kuwa na mambo yafuatayo:

1. Haki ya kuishi.

2. Haki ya kufanya maamuzi sahihi.

3. Afya bora. [Afya ni pamoja na mwili kutokushambuliwa na maradhi wala magonjwa; Akili kuwa na fikra nzuri; pamoja na uwezo wa kifedha!]

Yote hayo utayapata pale unapokuwa na maarifa. Soma vitabu vizuri, na ujifunze kwa waliofanikiwa. Hebu fikiri zaidi ya hapo awali; badili fikra zako. Usipende kuomba omba; jifunze kuwajibika kwenye maisha yako mwenyewe. Kila mtu anawajibika katika kuyabadili maisha yake yeye mwenyewe; iwe kiroho hata kimwili. Hakuna ajira itakayokufanya uwe tajiri, hakuna serikali itakayokufanya uwe tajiri; Hiyo yote ni mifumo tu! HAKUNA MFUMO ULIOTENGENEZWA ILI UKUFANYE WEWE UWE TAJIRI; kila mfumo umewekwa kumnufaisha zaidi yeye aliyeuweka! Kama wewe akili zako zote zinategemea ajira, au serikali ikuletee utajiri; basi elewa wazi umepata ziro katika mafanikio yako! Hata kama umeajiriwa, hebu waza kuwa na mambo yako mwenyewe. Hebu nikupe siri hii itakusaidia: Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing! Najua hapo wengi hawajaelewa, narudia tena: Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing! Narudia tena kwa mara ya tatu ili uelewe vizuri:

Dunia ya sasa imetoka katika mfumo wa kuajiriwa, bali imeingia katika mfumo wa Network Marketing!

Sio nia yangu hasa wakati huu kukufundisha what is Network Marketing or Direct Selling, or Personal Franchise, or Mult Level Marketing Business. Ukitaka kuyajua hayo nitafute kwa muda wako; lakini kama kweli unahitaji kufanikiwa; BADILI MTAZAMO NA FIKRA ZA AKILI YAKO.

Tunahitaji uhamsho katika kanisa; akili zilizokufa tunatakiwa tuzifufue. Hebu juilize; utakuwa omba omba mpaka lini? Nani kakwambia umasikini ni kutokana na elimu ndogo au kukosa mtaji! Ukweli ni kwamba; umasikini wa mtu umo katika fikra mbaya alizonazo.

Ongeza maarifa, acha kuomba omba, chukia umasikini lakini wapende masikini; wasaidie na uwaelimishe.

Jambo la mwisho ninalopenda kukwambia, ni hili: ONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU. Pasipo Roho Mtakatifu hauwezi kumpendeza Mungu, na pasipo kumpokea Yesu hauwezi kuurithi uzima wa milele. Kila ufanyalo zingatia HAKI na KWELI.

Nimeongea mengi lakini kwa uchache sana; yatakuwa na msaada kwake yeye mwenye hekima na akili. Mungu tayari amekwisha kukubariki, tatizo limo tu kwenye akili yako! Kumbuka kwamba:

UMASIKINI maana yake ni hali ya kukosa maarifa pamoja na kuwa na fikra / mtazamo mbovu akilini mwako! (POVERTY simply means; Lack of knowledge and having bad attitude! The state of having negative mentality).

Nawatakia baraka tele katika jina la Yesu Kristo. Amen.

Sunday, December 28, 2014

KUTII NENO LA MUNGU NA UTAKATIFU KWANZA.

KAMPENI YA UZIMA WA MILELE: 

"KUTII NENO LA MUNGU NA UTAKATIFU KWANZA."

Ukristo sio dhehebu; bali Ukristo ni mahusiano bora na Mungu.

Watu wengi hudhani Ukristo ni dhehebu ambalo limeanzishwa ili kuleta ustaarabu fulani katika jamii. Wakristo wengi wanaishi maisha ya kuigiza kisa tu ni wafuasi wa kanisa fulani! Wengine wanayaacha maagizo ya Mungu na kuyaheshimu mapokeo potofu ya dhehebu fulani eti kisa tu na wao wanajiita wakristo! Wengi wanaishi maisha ya maigizo, wanatenda dhambi kwa siri huku wakijiita "wapendwa"! Ndugu yangu na rafiki yangu; hapo unajidanganya wewe mwenyewe. Hakuna dhambi unayoweza kumficha Mungu. Leo ninasema na roho yako! Yachunguze matendo yako, chunguza siri za nafsini mwako; umemtenda Mungu dhambi. Umekuwa mnafiki, umekuwa na majungu japo unajiita mkristo, umekuwa mwizi japo unaitwa mpendwa, umekuwa mwongo umezaa hata nje ya ndoa yako kwa siri ukidhani Mungu hakuoni, umekuwa mshirikina na umejaa hila nafsini mwako. Unatenda ukidhani hakuna akuonaye; kumbe hapo wajidanganya wewe mwenyewe.
Biblia Takatifu inatuambia kwamba:

"Pumzi ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake." ~ Mithali 20:27.

Hakuna jambo uwezalo kumficha Mungu. Yeye anayajua mawazo yako hata kabla hujatenda jambo. Mungu anajua kuwa leo umekusudia kufanya uzinzi japo kuwa unamficha mchungaji wako! Anajua kuwa leo umetoka kufanya uzinzi japo kuwa unasema "Bwana Yesu asifiwe"!
Ichunguze nafsi yako, tubu sasa kwa maana neema bado ingalipo kwako. Wokovu sio wa maigizo, bali wokovu ni maisha halisi. Najua umeanguka mara nyingi dhambini lakini leo unayo nafasi ya kurekebisha maisha yako; Tubu sasa, la sivyo jehanam ipo kwa ajili yako na inakungoja.

Narudia tena kwa msisitizo: Ukristo sio dhehebu; bali Ukristo ni mahusiano bora na Mungu. Ukristo unaonekana katika kunena kwako, kuvaa kwako, upendo wako kwa Mungu na kwa majirani zako. Huwezi kusema Mungu hatazami uvaaji bali anatazama tu roho yako! Hapo hakika haupo salama; hicho ni kiburi tu cha uzima kinachokusumbua. Biblia inasema kuwa sisi ni barua isomwayo na watu wote (2 Kor 3:2), je ni tabia ipi uioneshayo kwa watu wasiomjua Mungu? Huko ni kuutukana wokovu wako, na hakika utatoa hesabu ya matendo yako yote. Haijarishi kuwa wewe unajiita au unaitwa mtume au nabii, haijarishi wewe ni mwinjilisti au mchungaji, haijarishi kwamba wewe ni mwimbaji au ni mwalimu, na hata kama wewe ni muumini wa kawaida tu; lakini nakuambia usipotubu leo, hakika kesho yako itakuwa ni ya majuto; itakuwa ni kilio na kusaga meno milele yote.
Biblia inapotuambia tujitenge na uovu wa kila namna (Zaburi 107:42); ni kwa sababu dhambi iingiapo unaweza ukaiona kama ni kitu kidogo tu, lakini usipoitubu na kuikemea utajikuta umejenga mazoea ya kuiona ni kitu cha kawaida tu; na hapo ndipo uovu unaumbika ndani yako. Hata kama ukikemewa utakuwa na kiburi kwa maana hiyo roho ya kuizoelea dhambi inakuandama. Dhambi sio kitu cha kuzoelea hata kidogo, dhambi imekusudia kukutenga tena na Mungu; uwe makini sana mpendwa. Leo ninaongea nawe kwa upole, ninaonge na roho yako. Rekebisha matendo yako kwa maana neema bado ingalipo kwako.
Biblia Takatifu inasema:

"Wanyofu wa moyo wataona na kufurahi, Na uovu wa kila namna utajifumba kinywa.
Aliye na hekima na ayaangalie hayo; Na wazitafakari fadhili za Bwana.
" ~ Zaburi 107:42-43

Mtu MNYOFU ndiye atakayeufurahia uzima wa milele; lakini mwovu atakataliwa mbali kabisa na Mungu. Kila jambo linayo kanuni yake, hata uzima wa milele pia unayo kanuni yake. Biblia Takatifu inatuambia kwamba:

"Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;
mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.
" ~ Waebrania 12:14-15

Tafuta kwa bidii amani kwa watu wote pamoja na huo UTAKATIFU. Tunapoelekea katika mwaka 2015, hebu kampeni yetu iwe ni "KUTII NENO LA MUNGU NA UTAKATIFU KWANZA" Tuyakemee na kujiepusha na mafundisho potofu.Tuzingatie hili:

"KUTII NENO LA MUNGU NA UTAKATIFU KWANZA"

Ukristo sio dhehebu; bali Ukristo ni mahusiano bora na Mungu. Nawatakia nyote baraka tele katika jina la Yesu Kristo, amen.

Thursday, December 25, 2014

UKWELI KUHUSU CHIMBUKO LA SIKU KUU YA CHRISTMAS.!

UKWELI KUHUSU CHIMBUKO LA SIKU KUU YA CHRISTMAS.!


Tusiwe wanafiki, tusiwe waongo! UONGO NI DHAMBI.

Mafundisho ya Yesu kazaliwa tarehe 25 Disemba yametoka wapi? Christmas sio sikukuu ya kusheherekea tarehe ambayo Yesu amezaliwa.
Tukitazama ushahidi wa Kibiblia hauoneshi Yesu alizaliwa mwezi gani wala tarehe gani; hata pia tukitazama ushahidi wa Kihistoria nao unatubainishia kuwa Yesu Kristo alizaliwa KATIKATI YA MWAKA 6 kwenda wa 5 b.C. Hivyo basi Yesu Kristo alizaliwa miezi ya KATIKATI YA MWAKA wala sio mwishoni mwa mwaka! Mambo haya ni muhimu sana kwako Mkristo uelewe, sio unakwenda tu kama kipofu.

Kwa ushuhuda wa kweli, katika Injili zote ndani ya Biblia Takatifu hakuna mahali po pote palipoandikwa kuwa Yesu Kristo alizaliwa majira yapi wala tarehe ipi; bali tunaona tu ushuhuda wa Yesu Kristo ambaye ni Mungu aliuvaa mwili kisha akazaliwa mfano wa mwanadamu! Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kunaelezwa wazi wazi katika Injili ya Mathayo 2:1-16, na katika Injili ya Luka 2:1-7. Tangu kuzaliwa kwa Yesu, hata wakati wa utoto wa Yesu, hata wakati wa huduma ya Yesu hapa duniani, hata wakati wa mitume, hadi kufika mwaka wa 349 AD hapakuwa na sherehe ya kuzaliwa kwa Yesu mnamo tarehe 25 mwezi Disemba kila mwaka!

JE, DESTURI HII IMETOKEA WAPI?

Mara nyingi tunapoelekea mwishoni mwa kila mwaka, tangu mnamo mwaka 350 AD, watu wengi duniani husherehekea siku kuu maarufu sana ijulikanayo kwa jina Christmas. Siku kuu hiyo huadhimishwa kila tarehe 25 ya mwezi Disemba kila mwaka, na wengi huamini kuwa ndiyo tarehe ambayo Yesu Kristo alizaliwa! Je, ni kweli kuwa Yesu alizaliwa katika tarehe hiyo (tarehe 25 Disemba)?
Kusema ukweli, kabla ya mwaka 350 AD, sherehe ya Christmas haikuwepo kabisa, na wala hapakuwepo na maadhimisho ya Yesu kuzaliwa katika tarehe 25 Disemba hadi ulipofika mnamo mwaka 350 AD wakati ambao papa wa kanisa la RC aitwae jina lake Julius I alipotangaza rasmi kuwa tarehe 25 Disemba ndiyo itakuwa siku ya kusheherekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo! Julius I alifanya hivyo kwa lengo la kuifuta na kuifidia siku ambayo wapagani walikuwa wakisherehekea kuzaliwa kwa “mungu” wao JUA na mwanzo wa majira ya “Spring” (kuchipuka kwa mimea).

Katika majira hayo ayo pia kulikuwa na sikukuu ya wapagani wa Kirumi inajulikana sana kwa jina la “Roman Saturnalia” ambayo pia Warumi walikuwa wanampa heshima “mungu” wao “Saturn” (sayari ya Satan), ambaye wao walikuwa wanamwabudu kuwa ndiye “mungu” wao wa mavuno! Warumi walikuwa wanaadhimisha sherehe hiyo kila mnamo tarehe 19 ya mwezi Disemba na ilikuwa inaadhimishwa kwa siku saba mfululizo hadi tarehe 25 ya mwezi huo wa Disemba ndipo maadhimisho ya siku kuu hiyo yalipositishwa.

Vivyo hivyo, katika Ulaya kaskazini, pia nao walikuwa wanaadhimisha sherehe ijulikanayo kwa jina la “Yule” ambayo pia waliifanya kwa heshima ya “mungu” wao kwa kuwa katika majira hayo ndipo wakati ambao majira ya baridi yalikuwa wanamalizika na jua lilianza kuchomoza.

Kimsingi na kiukweli maadhimisho ya siku ya Christmas HAYAMO ki Biblia, kwa sababu hayo ni mapokeo tu yaliyowekwa na wanadamu, na tena SIO TAHERE SAHIHI ambayo Yesu Kristo alizaliwa. Ndio maana yapo mataifa yanayoadhimisha kuzaliwa kwa Yesu mnamo mwezi Januari, na mengine wanaadhimisha miezi mingine kulingana na mtazamo wao; Bali hayo maadhimisho katika tarehe 25 Disemba yametokana na fundisho la Julius I wa kanisa la RC ambaye aliliweka kulingana na mitazamo yake yeye mwenyewe; japokuwa neno “Christmas” tukilinyambua tunapata jina “Christ - Mas” ambalo maana yake inakuwa “Christ” maana yake ni “Kristo”, na “Mas” huenda likawa na maana ya “Misa” japokuwa neno “Misa” lenyewe linakuwa linaandikwa “Mass” yenye double “ss” sio single “s”!

Huo ndio ukweli kuhusu chimbuko la sherehe ya Christmas katika tarehe 25 Disemba. Kwangu mimi binafsi Christmass ipo kila siku wala sio tu tarehe 25 Disemba kwa maana kila siku kwangu ni Ibada ya Kristo, pia ninajua kwamba Yesu HAKUZALIWA MWISHONI MWA MWAKA, bali Yesu Kristo ALIZALIWA KATIKATI YA MWAKA WA 6 kwenda MWAKA WA 5 b.C.

 Uthibitisho huo wa Yesu Kristo kuzaliwa mnamo KATI KATI ya mwaka wa 6 kwenda wa 5 b.C (k.K) pia unatibitishwa na Biblia ijulikanayo kwa jina la Life Application Study Bible, katika ule ukurasa wa "A20" kama jinsi picha hii inavyoonesha katika sehemu hiyo iliyozungushishwa duara jekundu.
Na kwa takwimu hizo, hata mwaka wa kwanza A.D (b.K) Yesu Kristo tayari alikuwa na umri wa miak mitatu unusu! Na hapo pia panapingana na ile dhana inayosemwa kuwa Yesu alipozaliwa ndipo miaka ikaanza kuhesabiwa kwa mfumo wa A.D.
Hilo fundisho la Yesu kuzaliwa tarehe 25 mwezi Disemba ni uongo tupu na ni lazima tulipinge kabisa, tena Kanisa la Kristo tunatakiwa kulipinga na kulipiga vita vikali kabisa.

Tuutafuteni wokovu sio kuitafuta tarehe ambayo Yesu alizaliwa; Kila siku tunapaswa kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu na thamani ya wokovu huu; sio tu katika tarehe 25 Disemba, bali kila siku tuwe katika uwepo wa Kristo. Mimi binafsi, kila siku kwangu ni Christ mass, hata leo pia. Tarehe haiokoi, bali Yesu ndiye anaokoa.


Je, wewe unasherekeaje Christmass?

TUMA KWA RAFIKI :

Twitter FacebookMore

 
Kuhusu Huduma Hii | Masharti Ya Utumiaji Wa Tovuti Hii | Wasiliana Nasi | Tangaza Kupitia Tovuti Hii